Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amesema kuwa huenda hali ikawa mbaya zaidi nchini humo kwani maambukizi ya virusi vya corona yanazidi kurekodiwa
Ramaphosa pia amesema kuwa atalegeza masharti ya kusalia nyumbani kuanzia mwezi Juni ila amewataka wananchi kuendelea na kuchukua tahadhari zinazohitajika.
Habari Nyingine: Familia yalishwa sumu kupitia chakula feki cha msaada cha Ruto, asema Kimani Ichung'wa
Kufikia sasa, nchi hiyo imethibitisha vifo vya watu 429 kutokana na Covid-19 huku ikikadiriwa na wanasayansi kuwa huenda watu zaidi ya 40, 000 wakapoteza maisha.
''Tutarajie kuwa na idadi kubwa ya watu walioambukizwa virusi vya COVID-19, janga la corona nchini Afrika Kusini litakuwa mbaya zaidi kabla ya hali kuwa nzuri,'' alisema Ramaphosa.

Habari Nyingine: Maafisa 4 wa KEBS wakamatwa kuhusiana na utapeli wa KSh.12 milioni
Aidha, Rais Ramaphosa alisema zaidi ya watu 164 katika kampuni ya madini nchini humo kwenye mgodi wa Mponeng wamekutwa na virusi vya corona.
Wagonjwa hao wote wametengwa na wanaendelea vema kiafya.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari zaidi TUKO.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjaoV6f5ZmmqiumZl6coWMoZiloV2Ws7O1yppkpK2jnruqecqurpplnZeuuq2Ms5iinJmWwKa5wGapmqGjYr%2BiucCpn6irkWO1tbnL